Jumatatu, 14 Julai 2014

Wawili wahofiwa kupoteza maisha

WATU WAWILI WAHOFIWA KUPOTEZA MAISHA BAADA KUFUNIKWA NA KIFUSI MKOANI KILIMANJARO by GLOBAL 13 minutes ago WATU zaidi ya wawili wanadhaniwa kupoteza maisha baada ya kufunikwa na kifusi wakati wakiendelea na shughuli za uchimbaji wa miamba kwa ajili ya uchongaji wa matofali. Tayari mpaka sasa mwili wa mtu mmoja aliyefahamika kwa jina Bless Adrian, mkazi wa kijiji cha Nganjoni wilaya ya Moshi vijijini mkoani Kilimanjaro umepatikana. Juhudi za kutafuta miili mingine inaendelea licha ya kukabiliwa na changamoto ya zana za kufukulia kifusi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni